20 May 2005

Huyu ndiye mwanamke wa shoka.

Sifa hizi za mwanamke wa shoka nimezipata katika maandiko matakatifu ya wakristo katika kitabu cha Mithali 31:10-31. Zinasema hivi:-

Mke mwema ni nani awezaye kumwona?
Maana kimachake chapita kima cha marijani.
Moyo wa mumewe humwamini,wala hatakosa kupata mapato.
Humtendea mema wala si mabaya, siku zote za maisha yake.
Hutafuta sufu na kitani,hufanya kazi yake ya mikono kwa moyo.
Afanana na merikebu za biashara,huleta chakula chake kutoka mbali.
Tena huamka kabla haujaisha usiku,
Huwapa watu wa nyumbani mwake chakula, na wajakazi wake sehemu zao.
Huangalia shamba akalinunua, kwa mapato ya mikono yake hupanda mizabibu.
Hujifunga nguvu viunoni kama mshipi, hutia mikono yake nguvu.
Huona kama bidhaa yake ina faida, taa yake haizimiki usiku.
Hutia mikono yake katika kusokota, na mikono yake huishika pia.
Huwakunjulia maskini mikono yake, naam huwanyooshea wahitaji mikono yake.
Hawahofii theluji watu wa nyumbani mwake, maana wote wa nyumbani mwake huvikwa nguo nyekundu.
Hujifanyizia mazulia ya urembo, mavazi yake ni kitani safi na urujuani.
Mume wake hujulikana malangoni, aketipo pamoja na wazee wa nchi.
Hufanya nguo za kitani na kuziuza, huwapa wafanyabiashara mishipi.
Nguvu na hadhi ndiyo mavazi yake, anaucheka wakati ujao.
Hufumbua kinywa chake kwa hekima, na sheria ya wema i katika ulimi wake.
Huangalia sana njia za watu wa nyumbani kwake, wala hawali chakula cha uvivu.
Wanawe huondoka na kumwita heri, mumewe naye humsifu na kusema,
Binti za watu wengi wamefanya mema, lakini wewe umewapita wote.
Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili,
Bali mwanamke amchaye Bwana ndiye atakayesifiwa.
Mpe mapato ya mikono yake, na matendo yake yamsifu malangoni.

0 Comments:

Post a Comment

<< Home