08 May 2005

Ngo...ngo...ngo..hodiii!

Ngo...ngo..ngo... hodiii, jamani wenyewe mpoo?...inaelekea wametoka, ngoja niache ujumbe mlangoni.

Wanablogu,
Nilipita kwenu lakini inaelekea hamkuwepo, nia hasa ilikuwa nikuwapa taarifa kwamba nami nimeingia katika ulimwengu wa blogu. Blogu yangu itajulikana kwa jina la Da'Mija, Da mija atakuwa akizungumzia masuala ya jamii na mabadiliko yake ya kila siku. Atafundisha atakapoona panafaa kufundisha, atajadili pale atakapoona panafaa kujadili, atatoa mawazo pale atakapoona panafaa kutoa mawazo na mengine mengi yatajitokeza kulingana na siku zitakavyokuwa zikienda.

Asanteni.


8 Comments:

At Sunday 8 May 2005 at 16:44:00 BST, Blogger Ndesanjo Macha said...

Karibu mwanakwetu!!!!

 
At Monday 9 May 2005 at 05:36:00 BST, Anonymous Anonymous said...

karibu sana , nasi tunasubiri kwa hamu kusoma mengi kutoka kwako

 
At Monday 9 May 2005 at 11:56:00 BST, Blogger Indya Nkya said...

Tunasubiri dada Minja usaidie katika jitihada za kuhabarisha jamii hasa wakati huu wa kujenga jamii habari

 
At Monday 9 May 2005 at 16:39:00 BST, Blogger Rama Msangi said...

haya ni mafanikio makubwa sana kwa wanawake wa Kiafrika ambao wanaanza kuona umuhimu wa kudhihirisha utamaduni wao na kujivunia popote waendapo. Karibu, karibu dada

 
At Monday 9 May 2005 at 16:54:00 BST, Anonymous Anonymous said...

Mh! umegonga kwa kasi sana kiasi tukaogopa kuwa tumevamiwa, si unajua tena watu walivyokata tamaa kuibuka na kukupiga roba za mbao sio jambo la ajabu kwahiyo mgeni akigonga lazima usikilizi anavyogonga kama anatumia FATUMA au laa. Karibu sana sisi tupo, karibu mgeni

 
At Monday 9 May 2005 at 18:38:00 BST, Anonymous Anonymous said...

Duuuu.... karibu mshirika ndo mambo hayo tunayotaka toka kwa ma dada zetu... Karibu Saaaana!

 
At Wednesday 11 May 2005 at 11:16:00 BST, Anonymous Anonymous said...

Da' Mija,

Hongera sana!

Fidelis Tungaraza.

 
At Thursday 26 May 2005 at 10:39:00 BST, Blogger Rama Msangi said...

nakushauri kuwa uweke kitabu cha wageni ndugu yangu

 

Post a Comment

<< Home