27 April 2006

Eti siku ya mtu kuzaliwa ni ya nani?..mama au mtoto?


Pichani juu ni mimi na kaka yangu na chini ni mzaa chema.

Hapo kipindi cha nyuma nilipata kuzua mjadala na mshairi maarufu wa kikundi cha Parapanda Mgunga mwa Mnyenyelwa juu ya hasa ni nani mwenye haki ya kuiita siku yake, je ni mama au mwana? kwa mujibu wa Mgunga anasema siku ya mtu kuzaliwa ni haki ya mama na kama ni sherehe au pongezi zote anayetakiwa kupewa ni mama. Hili nimelikumbuka leo kwa vile ni siku yangu ya kuzaliwa..., haya wewe unasemaje? ni nani anayetakiwa kupewa pongezi katika siku za kuzaliwa?

11 Comments:

At Thursday 27 April 2006 at 13:46:00 BST, Blogger MICHUZI BLOG said...

hepibethdei tu yuuu...X 3
hawoldayunaaauw....X 3
heeepiiiibethdaytu yuuuuuuu...X 1

jana tumesherehekea muungano, na hatukuwasherehekea nyerere na karume. mi nadhani bethdei ni siku ya mtoto...

 
At Thursday 27 April 2006 at 16:12:00 BST, Blogger Jeff Msangi said...

Naunga mkono kwamba siku hiyo ni ya mtoto.Mama alishawahi kupata yake kutoka kwa bibi wa mtoto.Ni siku ya mtoto.

 
At Thursday 27 April 2006 at 17:32:00 BST, Blogger mwandani said...

siku ni ya mtoto. Haswa kwa vile naona baba kasahauliwa. Mama na baba siku yao ni ile ilipotungwa mimba, au?

 
At Thursday 27 April 2006 at 19:35:00 BST, Blogger John Mwaipopo said...

Hepi bethidei tu yu. Siku ni yako.

 
At Friday 28 April 2006 at 08:50:00 BST, Blogger MK said...

Happy Birthday Damija! May God gives You 100 Years and more in Life.

Thanx,
©2006 MK

 
At Friday 28 April 2006 at 15:16:00 BST, Blogger mzee wa mshitu said...

WOW what a wonderful picture,Happy birthday to you Damija. Siku kwa hakika ni ya mtoto, mama atasherehekea nini wakati yake yamepita,au Mgunga anataka kusema mama anapojifungua anakuwa anazaliwa upya, sidhani. Ciao Happy to you!

 
At Sunday 30 April 2006 at 02:33:00 BST, Anonymous Anonymous said...

Mija;
Ikalaga na Mhola na Mulungu Agwinhe lubango lutaale uje gubutongi na buyegi bo shiku joose.

Nsizayo Ng'wanamatondo

 
At Sunday 30 April 2006 at 04:20:00 BST, Anonymous Anonymous said...

Heri ya siku ya kuzaliwa Da Mija. Uwe na maisha marefu (iwapo utakuwa unakula vizuri, kufanya mazoezi, tafakuri, n.k.).

Ndio miaka mingapi sasa? (naambiwa swali hili sio vizuri kuuliza wanawake!)

 
At Tuesday 2 May 2006 at 04:05:00 BST, Blogger John Mwaipopo said...

Mija ilikopigwa picha ya mzaa chema kuna uhusiano wowote na Kyela ama Kigoma hivi?

 
At Tuesday 2 May 2006 at 05:24:00 BST, Blogger Mija Shija Sayi said...

Asanteni woote kwa pongezi, naona zote zimenijia mimi na si mama. Hata mimi binafsi ninaamini siku hii ni ya mzaliwa sio mzaaji, maana kama ingekuwa hivyo basi baba yeye haki yake iko wapi? Mwandani umesema kweli juu ya hilo kwa upande wa baba.

Mwaipopo,
Hii picha sina hakika sana imepigwa wapi lakini kwa asilimia 99.8 ninaamini ni Mitaa ya Shinyanga au Mwanza.

Ndesanjo,
Kweli kabisa si vizuri kumuuliza mwanamke umri wake (sijui hata ni kwa nini) lakini mimi kiumri nimekuzidi mwaka mmoja haya piga mahesabu sasa hapo.

 
At Tuesday 2 May 2006 at 16:44:00 BST, Anonymous Anonymous said...

Hebu acha utani, umenizidi mwaka mmoja? Yaani ina maana hutakuwa ukinipa shikamoo. Hebu toka kule, acha utani.

 

Post a Comment

<< Home